Kijiwe cha KITIME
Thursday, May 16, 2013
Tuesday, April 30, 2013
VIDEO YA MAQUIS DU ZAIRE YA CHINYAMA , ENZI ZAO
Hawa ndio Maquis Du Zaire, wimbo huu, Kasongo, ulimletea
matatizo sana King Kiki ambaye ndiye aliyeutunga, maana serikali yake ya Kongo wakati huo Zaire ikiwa chini ya Mobutu Sese Seko iliuchukulia
kama ni fumbo fulani la kisiasa. Hii ilitokea kutokana na kuwa upande wa nchi anakotoka
Kiki, kulikuwa na upinzani wa daima na serikali ya Mobutu, japo mwenyewe Kiki anadai
wimbo huu haukuwa na uhusiano wowote na matatizo ya nchi yake.
-->
Hapa wanaonekana vigogo kama Chinyama Chiyaza (Baba yake Elly
Chinyama), Adios, Viking Nguza, King King, Kanku Kelly, Banza Mchafu na nyota wengine wengi
wa miaka hiyo. Mungu awalaze pema wote waliotangulia mbele ya haki
| Reactions: |
Friday, April 26, 2013
Wednesday, April 17, 2013
BI KIDUDE AFARIKI DUNIA...HISTORIA YAKE FUPI
Mwanamuziki mkongwe katika Taarab Fatuma Bint Mbaraka
maarufu kwa jina la Bi Kidude
amefariki dunia muda mchache uliopita huko Bububu Zanzibar, sehemu alikokuwa
anaugulia kwa kipindi sasa. Mwili wake utahamishiwa kwake Rahaleo na mazishi
yatakuwa kesho. Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo, alikuwa
binti wa mchuuzi wa nazi, hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe
ngapi, kuna hata mawazo kuwa alikwishafikisha miaka 102.
Katika mwaka
1920 tayari alikuwa amekwisha anza kuimba katika vikundi vya sanaa kule kwao,
mwaka 1930 alijiunga na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam na kuzunguka
miji mingi ya Tanganyika wakati ule , mwaka 1940 alirudi Zanzibar ambako awali
alikuwa amekimbia kwa kuwa aliozwa kwa nguvu na mtu aliyemzidi sana umri.
Bi Kidude pia liwahi kuimba na Sitti Binti Sadi wakati wa
ujana wake, na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote
akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni
Mungu Amlaze Pema Peponi Bibi yetu. Amen
| Reactions: |
Sunday, April 14, 2013
FELIX MANUAKU WAKU..BABA YA WAPIGA SOLO WA KONGO WA KIZAZI KIPYA
![]() |
| FRANCO |
![]() |
| FELLY |
Baada ya kuweka picha ya Franco akiwa kijana, mdau mmoja wa blog hii ametuletea taarifa hii..................
| Reactions: |
Sunday, April 7, 2013
KUMBE NYOTA NDOGO NI MTOTO WA MWANAMUZIKI WA JAMHURI JAZZ BAND
-->
![]() |
| Mzee Abdallah Hatibu (katikati) |
Nyota Ndogo ni jina maarufu sana Afrika Mashariki, ni mwanadada
mwanamuziki wnenye sauti tamu sana, kati ya vibao vyake vyote nikiri kuwa wimbo
wake wa Watu na Viatu ambao ulishinda tuzo katika Tanzania Music Awards 2007 ni wimbo ninaoupenda sana,
pia huyu binti ambaye amekwisha toa album kadhaa zikiwemo Chereko, Nimetoka
Mbali na Mpenzi alizaliwa 1981 na akapewa jina la Mwanaisha Abdallah.
Mwanaisha alizaliwa Mombasa hakumaliza shule na katika kazi alizopitia ni msaidizi wa
nyumbani. Katika kuonyesha tena kuwa wanamuziki wengine, muziki umo kwenye damu,
baba wa binti huyu alikuwa mwanamuziki. Katika maelezo ya rasmi ya Nyota Ndogo
baba yake alikuwa mwanamuziki wa bendi moja wapo Mombasa na aliitwa Abdallaha
Hatibu. Blog ya www.wanamuzikiwatanzania.blogspot.com
ambayo ni maarufu kwa kutafiti historia ya wanamuziki wa zamani wa hapa nchini
iliweka historia fupi ya kundi maarufu la Jamhuri Jazz Band, pamoja na picha ya
mmoja wa wanamuziki wa bendi hiyo aliyeitwa Abdallah Hatibu. Mwanamuziki mahiri
Profesa Abbu Omari aliyeko Japan ambaye pamoja na bendi nyingi alizopigia pia
alipiga Les Wanyika, na Simba wa Nyika alikuwa na maelezo ya ziada kuhusu Mzee
Abdallah Hatibu. Haya ndiyo aliyoyasema……Mkuu Kitime katika picha za hawa wakongwe wa Jamhuri jazz hapo kati kati
kuna mwanamuziki alikuwa anaitwa Abdallah Hatibu, sisi tulikuwa tunamjua kama
mzee Abdallah,alikwisha fariki miaka kama mitatu iliyopita,Huyu ni baba wa
waanamuziki wawili mashuhuri wa Mombasa mmoja msichana Nyota ndogo na mvulana
Juma Tutu, Mzee Abdallah alizikwa kwao Muheza baada ya kuishi Mombasa na
Nairobi kwa miaka mingi,hata mimi niliwahi kuishi nae jengo moja Nairobi 1982, Mzee
huyu alikuwa mkali kwa gitaa nadhani hata kushinda Michael Vicent, nadhani
huenda ikawa yeye ndiye aliyemfundisha Michael kupiga gita, niliwahi kumuuliza
kuhusu huyu Michael na akasema huyo alikuwa mtoto mdogo tu ki miziki kwake. Kwa
kweli huyu mzee Abdallah alikuwa mkali sana kwa gitaa Mombasa nzima na Nairobi
alijulikana. …..Abbu Omar Tokyo,Japan
![]() |
| Juma Tutu |
![]() |
| Nyota Ndogo |
Pia kadri ya website ya Juma Tutu , (JUMA TUTU) familia yao walizaliwa sita
sehemu ya Majengo huko Mombasa, baba yake alikuwa mpiga gitaa la solo katika
bendi ya Simba wa Nyika katika Club ya Sabasaba pale Mombasa, mama yao
Christine Mungala pia alikuwa muimbaji katika kwaya ya kanisani. Dada zake wawili Nyota Ndogo na Leila pia ni wanamuziki mahiri.
| Reactions: |
Wednesday, April 3, 2013
UNAUKUMBUKA WIMBO BB69? SIKILIZA HAPA
Ngaiyaoo Ngaiyaoo
Unipe mama, roho yangu
Nifurahi nayo, mpenzi wangu
Lakini sipendi kuchelewa bure
Wimbo huu nilipousikia mara ya kwanza kupitia santuri ulinigusa mahala ambapo mpaka leo umeacha nafasi fulani. Wimbo huu ulitungwa na Jeannot Bombenga na ukapigwa na na African Jazz group, African Jazz wakati huu ilikuwa imekimbiwa na yule mwamba wa muziki Afrika Grand Kalle ambae aliondoka na kundi Volcan Ni Beto Ba kwenda Ufaransa. Ilikuwa ni kama alama kuwa African Jazz ilikuwa inaweza kuendelea hata bila Mzee Kalle, huyu asije changanywa na Pepe Kaleni watu wawili tofauti sana.
| Reactions: |
Subscribe to:
Posts (Atom)





